Kituo cha
sheria na haki za binadamu nchini kimekutana na wasaidizi 64 wa kisheria kutoka
katika wilaya 28 nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo
katika utendaji wa majukumu yao ya kila siku ilikuwajulisha mabadiliko ya
sheria na pia sheria mpya.
Kutaniko
hilo huwa linafanyika mara kwa mara kila mwaka ikiwa ni kuwajengea uwezo
wasaidizi hao ili kuwa watendaji bora katika maswala ya kisheria nchini, Pia kutaniko
hilo lilikuwa na lengo la kumuaga aliyekuwa
mkurugenzi mkuu wa kituo cha hicho Dr. Hellen Kijo Bisimba ambaye anamaliza
muda wake kuwa Mkurugenzi mkuu wa kituo hicho.
Bi Hellen akiongea amesema
anafarijika kuona wasaidizi wa kisheria nchini wakiwa na shauku ya kuwasaidia
watanzania katika maeneo mbalimbali nchini ili kupata msaada wa kisheria
katika mazingira mbalimbali.
Bi Hellen aliongeza
kuwa amezidi kufarijika kuona kuwa vituo hivyo vya msaada wa kisheria nchini
katika wilaya mbalimbali vinazidi kuogezeka vikiwa na lengo la kuwasaidia
watanzania katika maswala mbalimbali ya kisheria.
Baadhi ya
wasaidizi wa kisheria kutoka Arusha na Manyara wamemwelezea Bi Hellen Kijo kuwa
alikuwa msaada sana kwao katika kipindi chake hivyo hawata weza kumsahau,baadhi
yao kwenda mbali zaidi kumwombea kwa Mungu afya nje na umri mrefu zaidi wa kuishi.
Bi.Anna
Henga ambaye ndiye mkurugenzi mpya wa kituo hicho cha sheria na haki za binadamu kwasasa
ambaye amempokea kijiti Bi Hellen amesema amepewa dhamana kubwa ya
kuendesha kituo hicho ila iko ndani ya uwezo wake hivyo amejipanga vizuri
kuweza kutimiza majukumu yake kwa uwezo wote kwa kushirikiana na watendaji wake
pia wasaidizi wa kisheria nchini kutimiza majuku ya kituo hicho.
![]() |
| Dr. Hellen Kijo Bisimba aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu akizungumza na wasaidizi wa kisheria kutoka wilaya 21 nchini. |
![]() |
| Bi.Anna Henga ambaye ndiye Mkurugenzi mpya wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu akizungumza na wasaidizi hao wa kisheria nchini |
![]() |
| Baadhi ya wasaidizi wa kisheria kutoka Arusha na ManyaraBaadhi ya wasaidizi wa kisheria kutoka Arusha na Manyara |
![]() |
| Wasaidizi wa kisheria kutoka wilaya zote nchini wakifuatilia mafunzo kwa umakini |
![]() |
| Wasaidizi wa kisheria kutoka wilaya zote nchini katika picha ya pamoja na aliyekuwa Mkurugunzi wa Kituo hicho Dr.Hellen Kijo Bisimba na Mkurugenzi mpya Bi Anna Henga. |
![]() |
| Wasaidizi wa kisheria kutoka wilaya zote nchini katika picha ya pamoja na aliyekuwa Mkurugunzi wa Kituo hicho Dr.Hellen Kijo Bisimba na Mkurugenzi mpya Bi Anna Henga. |






