Breaking News

Rais wa Uturuki: Tutajenga hospitali mbili kwa ajili ya kukabilia na virusi vya corona


Rais wa Uturuki asema kuwa   kutajengwa hospitali mbili mjini Istanbul kwa ajili ya kupambana na virusi vya corona.

Rais wa Uturuki Recep Tayyıp Erdoğan asema kuwa umechukuliwa uamuzi wa kujenga hospitali mbili  mabazo malengo yake ni kupambana na virusi vya corona.
Hospitali hizo zitajengwa mjini Istanbul.

Rais  Erdoğan ameyafahamisha  hayo baada ya kumalizika mkutano  ambao uligubika na hatau ambazo zinastahili katika makabailaino dhidi ya Covid-19.

Rais Erdoğan ameendelea kufahamisha kuwa hatua nyingine zitaendelea kuchukuliwa iwapo itahitajika kwa  kuwa hatua hizo malengo yake ni kupunguza  na kuzuia  maambukizi ya virusi vya corona.

Hospitali mbili zitajengwa karibu na uwanja wa ndege wa Atatürk  Yeşilköy na Sancaktepe, kila hospital moja itakuwa na vitanda  1000.

Ujenzi wa hospitali hizo unatarajiwa kumalizika baada ya siku 45.

Rais Erdoğan amesema kuwa  idara ya afya imefanya kila liwezekanalo  hadi kufikia idadi ya watu  20 000 kufanyiwa vipimo  katika muda wa siku moja huku akiendelea  kufahamisha  kuwa matibabu baada ya kugunduliwa waathirika  yatafanyika katika hospitali hizo mbili zinazotarajiwa  ujenzi wake kumalizika baada ya siku  45.


from MUUNGWANA BLOG https://ift.tt/2Xr4PIf

No comments