RC SHINYANGA AFANYA ZIARA YA UKAGUZI MIRADI YA MAENDELEO KISHAPU

Na Sumai Salum – Kishapu
  • ARIDHISHWA NA HATUA YA MIRADI YA MAENDELEO KISHAPU

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mboni Mhita, Julai 29, 2026 amefanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Kishapu mkoani humo, ikiwa ni pamoja na mradi wa sekta za elimu, afya, maji, miundombinu ya barabara, miradi inayotekelezwa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo pamoja na unufaishaji wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri. 

Akiwa katika ziara hiyo, Mhita amesema maendeleo yanayoonekana ni matokeo ya amani, utulivu na demokrasia ya kiuchumi inayowavutia wadau wa maendeleo na wawekezaji kushirikiana na Serikali kuboresha maisha ya wananchi.


Mhita amesema Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuwekeza katika sekta ya elimu kwa kujenga vyumba vya madarasa na kuboresha miundombinu ya shule ili kuhakikisha kila mtoto anapata haki ya elimu katika mazingira bora, ikiwa ni pamoja na kuongeza uwiano wa madarasa na matundu ya vyoo kulingana na idadi ya wanafunzi. Aidha, amepongeza vikundi vilivyonufaika na mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri, ikiwemo kikundi cha Wachapakazi kilichotumia mkopo huo kununua trekta kwa ajili ya kuongeza tija katika shughuli za uzalishaji.

Hata hivyo mmoja wa wananchi kutokea Kata ya Mwataga Patricia Nkana ameipongeza Serikali kwa kuendelea kuboresha huduma za afya na upatikanaji wa maji safi na salama, akisema ujenzi na uboreshaji wa zahanati na upanuzi wa upatikanaji wa maji safi na salama umeongeza usalama wa akina mama wajawazito wakati wa kujifungua na kuinua ustawi wa wananchi kwa ujumla na kuchochea kuimarisha afya ya ndoa zao.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Kishapu ikiwa ni pamoja na mradi wa sekta za elimu, afya, maji, miundombinu ya barabara, miradi inayotekelezwa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo pamoja na unufaishaji wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri Julai 29, 2026
Katibu Tawala mkoani Shinyanga Cp. Salum Hamduni akiwa kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Mboni Mhita Wilayani Kishapu Julai 29, 2026
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Mhe Peter Masindi akizungumza wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Mboni Mhita Wilayani humo ya kukagua miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na miradi ya sekta za elimu, afya, maji, miundombinu ya barabara, miradi inayotekelezwa kwa ushirikiano na wadau wa maendeleo pamoja na unufaishaji wa mikopo ya asilimia 10 ya Halmashauri Julai 29, 2026 Katibu Tawala wilayani Kishapu mkoani Shinyanga Fatma Mohamed akiwa kwenye ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Mboni Mhita Wilayani Kishapu Julai 29, 2026
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga Emmanuel Johnson
Mwananchi wa Kata ya Mwataga wilayani Kishapu mkoani Shinyanga Patricia Nkana akielezea namna wanavyonufaika na uboreshaji wa miundombinu hasa ya Elimu, Afya, Maji na Nishati ya Umeme hadi Vijijini Julai 29,2026 wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa huo Mhe Mboni Mhita wilayani humo

Tazama picha za matukio mbalimbali👇👇👇

























































































































































































from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/NgWLx84

Post a Comment

Previous Post Next Post