Makamu wa Rais Dk. Philip Isdori Mpango
Na Mwandishi Wetu
Makamu wa Rais Dk. Philip Isdori Mpango amewataka viongozi ambao wanatumia nafasi zao na maslaahi ndio wamekuwa wakichangia uharibu wa mazingira kwa asilimia kubwa taratibu zitafuatwa ni pamoja kupewa familia 12 zinazoharibu mazingira yetu
Dk.Philip Mpango ameyasema hayo wakati akifungua Kongamano la Wahariri na Wadau wa Uhifadhi , mazingira na Utunzaji wa Vyanzo vya Maji lililoandaliwa na Kituo cha Wanahabari, Watetezi wa Rasilimali na Taarifa (MECIRA) lililofanyika mkoani Iringa.
Dk. Mpango aliongeza kwa kusema "Lazima mazingira yapone na mazingira yabaki salama, viongozi wenye maslahi na kuweka rehani ya watanzania hawatakiwi"
Mpango amesema hayupo tayari kuona athari kubwa zinarudi kwa wananchi, na hivyo inatakiwa ushirikiano hasa kutoka katika serikali kuu wananchi, vyama vya siasa, vyombo vya habari, sekta binafsi na wananchi kwa ujumla na kuongeza kuwa kwa ushirikiano huo anaamini Nchi itashinda vita dhidi ya uharibufu wa mazingira ambao unaendelea.
Ametoa agizo kwa kwa Wakuu wa Mikoa kuhakikisha wanafanya mikakati ya utunzaji wa mazingira na pia amesisitiza kulilinda vyanzo vya maji katika mto Ruaha kwa nguvu zote, na pia nawakumbusha Wizara husika Mikoa pamoja na Taasisi husika kutekeleza maelekezo yaliotolewa na serikali ikiwa mi pamoja na kuweka alama za mipaka ya Utambuzi katika hifadhi.
Aidha Amewataka viongozi kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa waandishi wa habari katika kutoa elimu kwa jamii juu ya utunzaji wa mazingira.




