Bw. Habibu Mchange Mwenyekiti wa Kituo Cha Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na taarifa MECIRA akiwasilisha taarifa yake kwenye Kongamano la Wahariri na Wadau wa Uhifadhi, Mazingira na utunzaji wa vyanzo vya maji linalofabyika kwenye ukumbi wa Masiti Gangilonga Mkoani Iringa Leo Disemba 19,2022 ambapo Mgeni rasmi ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Philip Isdori Mpango.
Serikali
imeombwa kufanya maamuzi magumu ili kuokoa chanzo cha maji cha Bonde
la Ihefu ambalo limevamiwa na familia 12 na kusababisha chanzo hicho
kukauka.
Akizungumza
katika Kongamano la Wahariri wa Wadau wa Uhifadhi Mazingira na Utunzaji
wa Vyanzo vya Maji leo Desemba 19,2022 mkoani Iringa Mwenyekiti wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile amesema kuwa
inasikitisha kuona kwamba uharibifu wa mazingira ni wa kiwango cha juu
huku zikiwepo familia 12 zinazojinufaisha kupitia Bonde hilo wakiendelea
kukaliwa kimya.
Deodatus Balile Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF)
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile
Amesema
kuwa ameamua kutoa taarifa hizo hadharani licha ya ukweli kuwa anajua
wapo watu ambao hawatapenda kutokana na ukweli kuwa jambo hilo hata
watendaji wa Serikali wanajua ila wamefunga midomo.
Balile
amesema kuwa kama wahusika yaani watendaji wa Serikali hawatampatia
orodha ya majina ya familia hizo yeye yupo tayari kufanya hivyo ili
kunusuru chanzo hicho ambacho kinaendelea kutokea kwa sasa.
Mwenyekiti
huyo ameongeza kuwa familia hizo ndizo zinapaswa kunyweshwa sumu kabla
ya wengine kwa sababu wao ndio chanzo kikuu cha uharibifu huo kwa
makusudi kabisa wamekuwa wakifanya hivyo kwa manufa yao binafsi.
Awali
kabla ya Mwenyekiti Balile alizungumza Mwenyekiti wa wa Kituo cha
Wanahabari Watetezi wa Rasilimali na Taarifa Habibu Mchange alimwomba
sana Mh Dkt. Makamu wa Rais Dkt Mpango kuwa ili kuokoa na kulinda
rasilimali na vyanzo vya maji nchini vita hii inahitaji uchukuaji hatua
thabiti bila kumwonea aibu mtu.






