Rwanda kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kuelekea nchini Israel

Rwanda  inatarajia kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kuelekea nchini Israel.

Kwa mujibu wa gazeti la Israel la Yedioth Ahronoth,tangazo hilo limekuja baada ya mkutano kati ya waziri wa uchukuzi wa Israel Yisrael Katz na balozi wa Rwanda nchini Israel Joseph Rutabana.

Kulingana na makubaliano yaliyofanywa,Israel na Rwanda zitakuwa na safari saba za ndege kila siku kati ya uwanja wa ndege wa Ben Gurion wa Israel na uwanja wa ndege wa Kigali.

Rutabana amesema kuwa safari hizo zitaanza ndani ya miezi kadhaa ijayo.

Mnamo mwaka 2017,Israel ilifungua ubalozi wake kwa mara ya  kwanza nchini Rwanda.

from MUUNGWANA BLOG http://bit.ly/2RDgW2f

Post a Comment

Previous Post Next Post