UN walaani jaribio la mapinduzi nchini Gabon

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani vikali jaribio la mapinduzi nchini Gabon.

Msemaji Mkuu wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric katika mkutano wa waandishi wa habari amesema kuwa amepinga hatua ya jeshi kutaka kuipindua serikali nchini Gabon na kwamba huo ni uvunjaji mkubwa wa sheria.

Mapema Jumatatu asubuhi baadhi ya wanajeshi waliteka redio  ya taifa na kutangaza kuipindua serikali ya rais Bongo nchini Gabon.

Umoja wa Afrika nao umesikitishwa na hatua hiyo.

from MUUNGWANA BLOG http://bit.ly/2GXfkfw

Post a Comment

Previous Post Next Post