Breaking News

MATOLA: TUNACHUKUA POINTI 3 ZA SIMBA LEO - VIDEO

LICHA ya Simba kushinda mechi zake zote za hivi karibuni kwa kuanza na Mwandui 3-0, akafuata Mwarabu 1-0, African Lyon 3-0, Yanga 1-0 na Azam FC 3-1, kocha wa Lipuli, Selemani Matola amesema atawafunga Simba.

Simba itacheza kesho na Lipuli mchezo wa ligi ikiwa ni kiporo kwenye Uwanja wa Samora huku rekodi zikionyesha kwamba tangu msimu wa 2017/2018 Lipuli ilipopanda daraja, hakuna hata timu iliyoonja ushindi kwa mwenzake.

Matola alisema amewatazama wapinzani wake kwa ukaribu na kujua udhaifu wao, hali ambayo imemfanya aamini kwamba kesho atavunja rekodi iliyowekwa kwa timu hizi mbili.

Katika michezo hiyo mitatu ambayo walicheza nao msimu wa 2017/18 wakiwa nyumbani Simba walilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 kwenye Uwanja wa Samora, mchezo wa marudiano Lipuli walilazimisha sare ya bao 1-1 Uwanja wa Taifa.

Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza msimu huu, zilitoka suluhu Uwanja wa Taifa.



from SALEH JEMBE

No comments