Breaking News

Naibu Waziri, Subira Mgalu amkalia kooni Mkandarasi


Na. Ahmad Mmow,Lindi

Naibu waziri wa Nishati, Subira Mgalu ametoa wiki moja kwa mkandarasi wa ujenzi wa miundombinu ya umeme,kampuni ya State Grid  Electrical and Technical Works kumaliza kazi ya kuunganisha umeme katika vijiji vya Mtama baada ya kuchelewa kumaliza kazi hiyo kwa takribani miezi sita.

Mgalu alitoa agizo hilo baada ya baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mihogoni kumlalamikia kuhusu kuchelewa  kuunganishwa umeme katika vijiji vyao.

Wananchi hao walisema  kuchelewa kwa mradi wa  umeme katika eneo lao kunasababiswa na uzembe wa mkandarasi anayejenga mradi huo.

Walisema ni vyema serikali ikaangalia uwezekano wa kubadilisha makandarasi ili mradi huo ukamilike kwa wakati

Baada ya kusikia malalamiko na maombi ya wananchi hao, Mgalu alisema serikali haiwezi kuwavumilia watendaji au wakandarasi wanaofanya kazi kwa mazoea. Kwahiyo mkandarasi huyo akamilishe zoezi la kupanda nguzo za umeme na kuwasha ndani ya siku saba alizompa.

Alisema  serikali inatambua umeme ni biashara sio anasa,hivyo  vijiji 30  vilivyopo kwenye mpango katika wilaya Lindi na 133 vya mkoa wote wa Lindi vitapate umeme.

Kwa upande wake, Meneja Mradi wa kampuni ya  State Grid Electrical and Technical Works Mhandisi, Bahati Manyangali alikiri kuwepo kwa ucheleweshaji  wa umalizaji wa kazi hiyo.Hata hivyo alisena uchelewaji huo ulikotokana na sababu za kiufundi na kuchelewa  nguzo za umeme

Alisema tayari kazi ya kupanda nguzo 10  kati ya 30 zinazotakiwa kupandwa katika kijiji cha Mihogoni  imeanza.



from MUUNGWANA BLOG https://ift.tt/2VsY44l

No comments