Breaking News

Yondani asifu kiwango alichoonyesha Kindoki


Beki mkongwe wa Yanga SC, Kelvin Yondani amesifu kiwango kilichoonyeshwa na kipa wa timu hiyo Klausi Kindoki huku akimtaka kutobweteka.

Yondani ameongea hayo ikiwa ni siku  tangu kipa huyo aonyeshe kiwango kikubwa cha kuokoa michomo ya Namungo FC katika mchezo wa Kombe la Shirikisho ambao ulimalizika kwa Yanga kushinda bao 1-0 lililofungwa na Heritier Makam­bo.

Yondani amesema kuwa Kindoki ni kipa mzuri mwenye uwezo mkubwa wa kudaka, lakini presha ya mashabiki ndiyo imemfanya apoteze hali ya kujiamini akiwa golini.

“Kindoki siyo kipa mbaya ni mzuri na nilianza kumuo­na tangu alipojiunga na Yan­ga mwanzoni mwa msimu huu, kosa kubwa alilolifanya aonekane siyo mzuri ni kupoteza hali ya kujiamini baada ya kufungwa mich­ezo ya mwanzoni, lakini sasa amesha­waonyesha watu kuwa yeye ni hatari sana.

Hata hivyo ameongeza kuwa anachotakiwa ni kuwajua mashabiki na kuongeza hali ya ku­jiamini ili akontroo presha kama alivyofanya katika mchezo uliopita wa Kombe la Shirikisho walipocheza na Namungo, kiukweli alidaka vizuri.





from MUUNGWANA BLOG https://ift.tt/2BV55nf

No comments