Breaking News

GAVANA SHILATU ASHIRIKI UJENZI ZAHANATI ‘NI ULE ALIOAGIZA UENDELEZWE’


Na Mwandishi wetu Mihambwe 

Afisa Tarafa Mihambwe Gavana Emmanuel Shilatu ameshiriki ujenzi wa Zahanati ya Ngongo iliyopo Kijiji Cha Ngongo kilichopo kata ya Michenjele.
Gavana Shilatu alienda kufuatilia utekelezaji wa maagizo yake ya ujenzi wa mradi huo wa Zahanati alioagiza ndani ya siku mbili uanze kutokana na kutelekezwa tangu Mwaka jana. 

Gavana Shilatu alifurahishwa kukuta nyasi zimefyekwa na Mafundi wapo kazini Kama alivyoagiza na kuwasisitiza watangulize mbele uzalendo kwa kuhakikisha mradi unajengwa kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyolingana na thamani ya pesa. 

Katika ushiriki wa ujenzi huo Gavana Shilatu aliambatana na Serikali ya Kijiji pamoja na kamati ya ujenzi.



from MICHUZI BLOG

No comments