Breaking News

Iraq, Iran kuimarisha ushirikiano wa biashara na uwekezaji


Viongozi wa Iraq na Iran wamekutana na kufanya mazungumzo Jumatatu mjini Baghdad na kufikia makubaliano, pamoja na mambo mengine, kuimarisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili, katika nyanja za biashara, na uwekezaji.

Shirika la Habari la AFP limesema nchi hizo zinaangaza kuimarisha ushirikiano wa pamoja katika nyanja zote, kama vile ushirikiano wa kibiashara, maeneo ya uwekezaji, kuanzisha miji ya viwanda ya pamoja, biashara ya mpakani, ushirikiano wa utalii kati ya nchi hizo mbili.

Maeneo mengine ni ziara baina ya wananchi wa Iran na Iraq, ushirikiano katika nyanja za nishati, gesi, umeme, mafuta, benki, huduma za kiufundi na uhandisi na maeneo ya barabara na reli, maji. Pia masuala mengine husika ni mazingira na masuala ya kitaifa na kimataifa..

Rais wa Iran Hassan Rouhani amewasili Baghdad Jumatatu, televisheni ya Iraqi imesema, akiwa katika ziara yake rasmi ya kwanza kwa taifa hilo ambayo Tehran iliwahi kupigana vita vilivyomwaga damu dhidi ya nchi hiyo na baadae hivi sasa inapambana na kikundi cha Islamic State.

from MUUNGWANA BLOG https://ift.tt/2VSBHFK

No comments