Breaking News

LEO NDIYO LEO! TUZO ZA SAMIA KALAMU AWARDS 2025 ZINATOLEWA! MGENI RASMI MHE. RAIS SAMIA!!

 
Waandishi wa habari kutoka kila pembe ya Tanzania leo  Mei 5,2025 wanakutana katika Ukumbi wa Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam kuanzia saa 11 Jioni kwa tukio kubwa na la kihistoria – Samia Kalamu Awards 2025.

Hii ni siku maalum ya kutambua, kuthamini na kuenzi mchango wa wanahabari katika maendeleo ya taifa, ambapo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.

Kaulimbiu ni #UzalendoNdoUjanja, ikihamasisha wanahabari kutumia kalamu zao kwa weledi, maadili na uzalendo wa kweli kwa taifa.

Tuzo hizi zinalenga kutoa motisha kwa wanahabari wanaofanya kazi kwa bidii na ubunifu katika nyanja mbalimbali kama vile habari za uchunguzi, makala bora na habari za maendeleo.

Kwa picha na matukio yanayojiri:
Habari zaidi:




from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/1bhGvxg

No comments