Breaking News

MKUU WA SOKO KUU ARUSHA AJITOSA UBUNGE JIMBO LA LUDEWA




Katika hatua za mwisho za mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkuu wa Soko Kuu la Arusha, Ndugu John Haule, amejitokeza kuchukua na kurejesha fomu ya kuomba ridhaa ya chama hicho kugombea Ubunge wa Jimbo la Ludewa mkoani Njombe.

Haule amefika katika Ofisi za CCM Wilaya ya Ludewa Julai 2,2025 ambapo amesema amepata ushirikiano mkubwa kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya pamoja na viongozi wengine wa chama.

"Ushirikiano nilioupata umenipa moyo zaidi, na ninayo nia ya dhati kulitumikia Jimbo la Ludewa kwa weledi na uzalendo," amesema Haule.

Ikumbukwe kuwa mwaka 2022, Ndugu John Haule aliwahi pia kuonesha nia ya kugombea Ubunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA).



from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/5pxkbTM

No comments