SAKALA AINGIA KWENYE KINYANG'ANYIRO UDIWANI KATA YA MJINI - SHINYANGA
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini Abdulaziz Said Sakala (kulia)akikabidhi Fomu ya Udiwani Kata ya Mjini,kwa Katibu wa CCM Kaya hiyo Rashid Abdalla.
Na Marco Maduhu,SHINYANGA
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini Abdulaziz Said Sakala,amerejesha Fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Udiwani Kata ya Mjini kwenye uchaguzi Mkuu 2025.
Amerudisha Fomu hiyo leo Julai 3,2025, kwenye Ofisi za Chama Cha Mapinduzi CCM Kata ya Mjini.
Akizungumza mara baada ya kurudisha Fomu hiyo,amesema akipata ridhaa ya kuwa Diwani atawaletea maendeleo wananchi,na kwamba mengi atayazungumza pale jina lake litakapoteuliwa.
"Katika uchaguzi huu,nafarijika kuona vijana wengi wamejitokeza Kugombea nafasi ya Udiwani na Ubunge, na pia nakishukuru Chama changu kwa kudumisha demokrasia," amesema Sakala.
from MALUNDE 1 BLOG https://ift.tt/DdUMKmP
No comments